Monday, December 3, 2012

Mgao wa umeme wairudisha TANESCO katika usukukani wa kero




Uchunguzi uliofanywa na wanahabari katika zoezi la kukusanya kero za sekta binafsi linaondelea kupitia mitandao ya jamii ya Twitter na Facebook umeonyesha kuwa wakazi wa jijini Dar es Salaam wanakabiliwa na mgao wa umeme kwa kipindi kirefu sasa.
Hali hiyo imebainika wakati wa majumuisho ya kero za wateja wa huduma na bidhaa mbalimbali nchini Tanzania  katika mzunguko wa tatu ambapo Shirika la Ugavi wa Umeme TANESCO limechukua nafasi ya kwanza kati ya biashara 36 zilizotajwa kuwa kero kwa wateja.
Jumla ya kero tofauti 220 zimewasilishwa na wateja toka zoezi hilo lianze ambapo Shirika la Tanesco lina jumla ya kero 71 ambapo kati ya hizo 60 ni kutoka Dar es Salaam pekee.
Katika mzunguko huu  nafasi ya pili ilishikiliwa na Kampuni ya Mawasiliano ya Tigo yenye kero 63 kati ya 220  huku nafasi ya tatu ikiwaendea  Kampuni ya Mawasiliano ya Vodacom yenye kura 17 kati ya 220 zilizowasilishwa.  

No comments:

Post a Comment